Baba Mtakatifu Francisko ameridhia uteuzi wa Kardinali Joao Brazi de Aviz kuendelea
kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume pamoja
na kuteuwa baadhi ya wajumbe wapya kwenye Baraza hili. Papa pia ameridhia uteuzi wa
Kardinali Jean Louis Tauran na Padre Miguel Angel Ayuso Guixot kuwa ni Rais na Katibu
mkuu wa Baraza la Kipapa na Majadiliano ya Kidini pamoja na kuwateua baadhi ya wajumbe
wapya ili kuongeza nguvu katika majadiliano ya kidini.
Wakati huo huo, Baba
Mtakatifu Francisko ameridhia uteuzi wa Kardinali Gianfranco Ravasi, Askofu mkuu Carlos
Alberto de Pinho Moreira Azevedo pamoja na Askofu mkuu Barthèlemy Adoukonou kuwa ni
Rais, Mwakilishi na Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la Utamaduni.