2014-03-29 11:07:14

Familia imepewa dhamana ya kutunza uhai na kuelimisha utunzaji bora wa mazingira!


Baraza la Kipapa la Familia kwa kushirikiana na Kikundi cha Greenaccord, Jumamosi, tarehe 29 Machi 2014 limefanya semina maalum kuhusu mchango wa Familia katika utunzaji wa mazingira, uliowashirikisha viongozi wa Makanisa, Serikali, Wachumi na Watetezi wa mazingira. Imekuwa ni fursa pia ya kusikiliza ushuhuda uliotolewa na Familia moja kutoka Napoli, kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira pamoja na kuanza mchakato wa maisha yanayoenzi utunzaji bora wa mazingira.

Baba Mtakatifu Francisko kwa kutambua umuhimu na ushiriki wa Familia katika utunzaji bora wa mazingira ametuma ujumbe kwa washiriki wa semina hii, kwa kusema kwamba, Familia kimsingi ni mahali maalum pa kutoa hifadhi ya zawadi ya uhai na elimu makini kwa ajili ya kulinda na kutunza kazi ya uumbaji ambayo mwanadamu amekabidhiwa kwa ajili ya mafao ya sasa na kwa ajili ya kizazi kijacho.

Ujumbe wa Baba Mtakatifu umeandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, katibu mkuu wa Vatican anayekazia umuhimu wa kutunza mazingira kwa ajili ya mafao ya wengi. Baba Mtakatifu anawatakie washiriki wote wa semina hii heri na baraka zake za kitume.







All the contents on this site are copyrighted ©.