Baada ya viongozi wa Kanisa kufanya uchunguzi wa kina kuhusu tuhuma za ubadhirifu
wa mali ya Kanisa uliofanyika Jimbo Katoliki la Limburg, Ujerumani, imeamriwa kwamba,
Askofu Franz-Peter Tebartz-Van Elst, hana tena sifa za kuweza kuongoza Familia ya
Mungu Jimboni humo.
Vatican imekubali ombi la kung'atuka kutoka madarakani
lililowasilishwa na Askofu Franz-Peter na hivyo, Askofu Manfred Grothe ameteuliwa
kuwa Msimamizi wa Kitume. Baba Mtakatifu anaiomba Familia ya Mungu Jimboni humo kuupokea
uamuzi huu kwa moyo mkunjufu na kwamba, Askofu Tebartz-Van Elst, atapangiwa kazi nyingine.