2014-03-25 08:10:39

Jitahidini kuwa ni vyombo vya haki, amani na upatanisho wa kweli!


Kuna haja kwa waamini na wananchi wa Senegal katika ujumla wao kuanzisha mchakato wa umoja, udugu na upatanisho wa kitaifa baada ya watu kupata majeraha makubwa ya machafuko ya kisiasa nchini humo ambayo yamedumu kwa kitambo kirefu.

Ni ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko kwa wananchi wa Senegal, ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican wakati waamini wa Senegal walipokuwa wanafanya hija ya ishirini na sita, kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa Tèmento. Baba Mtakatifu anasema, wananchi wameathirika sana kutokana na kinzani na migawanyiko, changamoto ya kuanza ukurasa mpya wa maisha kwa kujikita katika kweli za Kiinjili na sala bila ya kukata tamaa ili kumwomba Mwenyezi Mungu awawezeshe wananchi wote kuwa ni vyombo vya amani na upatanisho.

Ujumbe wa Baba Mtakatifu umesomwa Jumapili iliyopita, tarehe 23 Machi 2014 na Askofu mkuu Mariano Montemayor, Balozi wa Vatican nchini Senegal wakati wa Ibada ya Misa Takatifu kwa mahujaji waliokuwa wamefurika kutoka katika majimbo kadhaa nchini humo.







All the contents on this site are copyrighted ©.