Matumaini ni fadhila ya Kimungu inayomwezesha mwamini kutamani heri ya Ufalme wa mbinguni
na uzima wa milele, kwa kutumainia ahadi za Kristo na kutegemea, siyo nguvu zao, bali
msaada wa neema ya Roho Mtakatifu. "Na tulishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke;
maana Yeye aliyeahidi ni mwaminifu".
Fadhila ya matumaini inajibu tamaa ya
heri iliyowekwa na Mungu katika moyo wa kila mtu. Yachota matumaini yanayovuvia matendo
ya watu. Huyatakasa ili kuyapanga kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni nyakati za upweke.
Hufungua moyo katika kungoja heri ya milele. Akielekezwa na matumaini anakingwa na
ubinafsi na anaongozwa kwenye furaha itokanayo na upendo.
Baba Mtakatifu Francisko
katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anawakumbusha kwamba, Yesu
ndiye tumaini lao. Hakuna kitu chochote iwe mateso au kifo kinachoweza kuwatenganisha
nguvu ya upendo wa Mungu unaookoa.