Ugonjwa na mateso yamekuwa daima kati ya matatizo mazito sana yanayoweka maisha ya
mwanadamu katika majaribu. Katika ugonjwa mtu anapata mang'amuzi ya kutokuwa na uwezo,
ya mipaka yake na kikomo chake. Kila ugonjwa unaweza kutufanya tuchugulie kifo.
Ugonjwa
waweza kutupeleka kwenye uchungu, kujihangaisha wenyewe, pengine hata kukata tamaa
na kumwasi Mungu. Waweza pia kumkoza mtu zaidi, kumsaidia kupambana katika maisha
yake kile ambacho si cha lazima ili kuelekea kile kilicho cha lazima na muhimu katika
maisha. Mara nyingi sana ugonjwa huchochea kumtafuta Mungu na kurudi kwake.
Baba
Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema
kwamba, ugonjwa na kifo si mwiko. Huu ni ukweli ambao watu wanapaswa kuukumbatia mbele
ya Yesu.