Rais Filip Vujanovic akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 20 Machi 2014 amekutana na kuzungumza na
Rais Filip Vujanovic kutoka Montenegro na baadaye alikutana pia na kuzungumza na Kardinali
Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique
Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.
Katika
mazungumzo kati ya Baba Mtakatifu na mgeni wake, kwa pamoja wameridhika kwa hali ya
uhusiano kati ya Vatican na Montenegro pamoja na kuonesha nia ya kutaka kuimarisha
zaidi uhusiano kati ya Kanisa na Serikali kwa ajili ya mafao, ustawi na maendeleo
ya wananchi wa Montenegro. Viongozi hao wamegusia pia masuala ya kimataifa na kikanda
pamoja na kuangalia mchakato wa Montenegro katika harakati za kutaka kujiunga na taasisi
za Jumuiya ya Ulaya.