2014-03-18 10:20:17

Papa Francis: njia ya amani ni kupitia huruma


Vatican Radio) Ili kupata huruma ni lazima kwanza ya kusamehe . Ni kwa njia ya msamaha kwamba mioyo yetu , na dunia , hujazwa na amani . Ni maudhui ya Papa Francisko katika homilia yake ya wakati wa Ibada ya Misa Jumatatu asubuhi, katika kanisa dogo la Mtakatifu Marta la ndani ya Vatican.

Papa alieleza kwa kurejea maneno ya Yesu kwa wafuasi wake aliposema, "Kuweni na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma" . Papa alionyesha kutambua kwamba ,pengine siyo rahisi kuielewa hii tabia ya huruma kwa sababu tumezoea kuhukumu. Na kwamba wengi tunakosa kuelewa maana ya huruma kwa kuwa hatuna asili hiyo ya kusamehe.

Na ili kuwa na huruma, Papa aliendelea, kuna mambo mawili yanayohitajika. Kwanza ni elimu ya mtu mwenyewe . Elimu hii binafsi ina maana ya kukiri kutenda jambo baya ! Na hivyo kujiona ni mwenye dhambi, na hivyo kuiona haja ya kutubu na kuiungamia haki ya Mungu, ambayo ina uwezo wa kumbadilisha mtu kwa huruma na msamaha wake. Na hivyo, lazima tuone aibu kwa dhambi zetu na kuomba huruma ya Mungu .

Papa aliendelea kufafanua kwamba “si lazima kutenda dhambi kubwa kama kuua mtu , lakini kuna mambo mengi madogomadogo ambamo tunatenda dhambi, na dhambi ni nyingi kila siku, na mtu anapaswa kuiona roho yake ni dogo kubeba dhambi zote na hivyo anapaswa kuona aibu mbele za Bwana na mbele ya Mungu, na mbele ya wengine na hivyo kuomba msamaha. Inaonekana kama ni rahisi, lakini ni vigumu sana kusema, Nimekosa”.

Papa aliendelea kuonya kwamba, mara nyingi, ni vyepesi sana kuwalaumu wengine kwa ajili ya dhambi zetu, kama alivyo walivyo fanya Adamu na Hawa. Ni rahisi kumsingizia mtu mwingine, kwamba ndiye chanzo cha kutenda dhambi , lakini dhambi hiyo umeitenda mwenyewe! Na iwapo tunapata utambuzi huo kwamba, tumetenda dhambi na kuomba msamaha kwa unyenyekevu kwa sababu tunajisikia ndani mwetu kumkosea na tunahitaji huruma ya Mungu, vivyo hivyo kama tunavyosali katika sala ya Baba Yetu : "Utusamehe , kama sisi tunavyo samehe waliotukosea, ni lazima iwe hivyo, kuwa na huruma kwa wengine kabla hatujaomba huruma ya Mungu kwa dhambi zetu.

Tabia nyingine tunahitaji kuwa nayo ili kuipata huruma ya Mungu , Papa aliendelea, ni kuwa na moyo mpana, kwa sababu moyo mdogo ni moyo wenye ubinafsi usio weza kuwa na huruma .

Moyo na huruma, alisema Papa Francis, " hauna lawama , lakini husamehe na kusahau, kwa sababu Mungu husahau dhambi zetu, Mungu hutusamehe dhambi zetu na hivyo moyo hupanuka. Hili ni jambo nzuri , Papa alisema:” Wewe ni mwenye huruma " .

Watu wenye huruma, wanawake kwa waume ni wale wenye mioyo mipana, ambao daima husamehe wengine na kufikiri juu ya dhambi zao wenyewe. Hii ni njia ya huruma ambayo ni lazima kila mmoja aiombe. Papa amesisitiza na kuhoji “kwa jinsi gani dunia ingekuwa ni dunia ya amani iwapo watu wote, kama mtu binafsi, familia na vitongojini ,wangekuwa na tabia hii. Na kwa jinsi gani amani ingekuwa mioyoni mwetu! Kwa sababu huruma huleta amani. Daima tunapaswa kukumbuka :' Mimi ni nani kuhukumu ? Kuwa na aibu na kupanua moyo wako. Bwana na atujalie neema hii







All the contents on this site are copyrighted ©.