Matashi mema ya watu wa Argentina yawalishwa rasmi kwa Papa
Vatican Radio) Jumatatu Katika jengo la “Domus Santa Marta”, Papa Francisko alimpokea
Rais Cristina Fernandez de Kirchner, Rais wa Jamhuri ya Argentina. Rais de Kirchner
aliyekuwa amefuatana na ujumbe wake rasmi .
Hii haikuwa mara ya kwanza kwa
Kiongozi huyo wa Argentina kukutana na Papa Francisko, kwa kuwa alikutana naye mara
ya kwanza tarehe 18 Machi 2013, siku moja kabla Ibada ya Uzinduzi wa utume wake
kama Papa. Na pia alikutana na Papa tarehe 28 Julai 2013, wakati wa Ibada ya Misa
ya kuhitimisha Siku ya Vijana Duniani iliyofanyika Rio de Janeiro, Brazil.
Lengo
la ziara ya Jumatat, ilikuwa kuwasilisha kwa Baba Mtakatifu Francisko, salamu
na nia njema za watu wa Argentina, kwa ajili ya tukio la maadhimisho ya mwaka mmoja
kupita tangu raia mwenzao wa Argentina, kuchaguliwa kuwa Papa .