2014-03-18 07:53:29

Endeleeni kusali kwa ajili yangu na Kanisa!


Baba Mtakatifu Francisko tarehe 13 Machi 2013 alichaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki, kwa unyenyekevu na moyo mkuu akaanza utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro, huku akizungukwa na bahari ya sala na sadaka iliyokuwa inatolewa na watu mbali mbali ndani ya Kanisa.

Katika Maadhimisho ya Siku kuu ya Mtakatifu Yosefu mchumba wake Bikira Maria na Msimamizi wa Kanisa, Baba Mtakatifu Francisko, hapo tarehe 19 Machi 2013 akaanza rasmi kuliongoza Kanisa kwa Ibada ya Misa Takatifu iliyoadhimishwa kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa viongozi wa Kanisa, Serikali na Dini mbali mbali.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, anapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa wote wanaomkumbuka kwa sala na matashi mema wakati huu anapoadhimisha Mwaka mmoja tangu alipochaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki. Anawasihi kuendelea kusali kwa ajili yake na Kanisa kwa ujumla.







All the contents on this site are copyrighted ©.