Papa na wasaidizi wake warejea kutoka Mlimani kwa sala na mafungo!
Baba Mtakatifu Francisko amemshukuru Monsinyo Angelo de Donatis, Paroko wa Parokia
ya Marko Mwinjili, Jimbo kuu la Roma, aliyeongoza mafungo ya kiroho kwa Papa pamoja
na wasaidizi wake wa karibu.
Baba Mtakatifu
anasema, mafungo haya yamekuwa ni msaada mkubwa katika hja ya maisha yao ya kiroho.
Wamepewa mbegu ya Neno la Mungu itakayotunzwa na Yesu mwenyewe kwa kuipatia mvua ya
kutosha hadi itakapozaa matunda yanayokusudiwa.
Baba Mtakatifu anasema, Padre
De Donatis amekuwa ni nguri wa kupandikiza mbegu ya Neno la Mungu, kazi ambayo ameifanya
kwa umakini mkubwa pamoja na kuhakikisha kwamba, lengo linafikiwa. Baba Mtakatifu
anamwomba Monsinyo De Donatis kuwakumbuka na kuwaombea “viongozi na waamini hawa”
ambao hata katika mapungufu yao ya kibinadamu bado wana ari na moyo mkuu wa kutaka
kumfuasa Yesu Kristo kwa karibu zaidi, huku wakiwa na matumaini katika ahadi zake
na kwa furaha zaidi.
Baba Mtakatifu tayari amekwisharejea mjini Vatican baada
ya kwenda jangwani kwa takribani juma zima, tayari kuendelea na utume wake, akiwa
amesheheni nguvu ya Roho Mtakatifu.