2014-03-07 09:27:27

Kama hatusameheani makosa si wafuasi wa Yesu


Kardinali James Francis Stafford, Mkuu mstaafu wa Idara ya Kipapa ya kitubio , ametoa tafakari juu umuhimu na maana ya kupokea huruma ya Mungu wakati huu Mama Kanisa anapokianza kipindi cha Kwaresima. Anasema, kipindi cha Kwaresima daima ni wakati ambamo Kanisa zima: Wakatekumeni, na walimu wao, wadhamini, makatekista, Parokia - Kanisa zima, hutafakari kwa makini huruma ya Mungu.

Amefafanua kwamba, huruma ya Mungu lazima iwe hai katika maisha yetu binafsi kama Mkristo na pia maisha ya jamii zima ya waamini wa Kristo. Ni wakati wa kuiishi huruma ya Mungu kimatendo, katika maana ya kusameheana mmoja kwa mwingine. Kama Mkristu binafsi au jamii ya kanisa hailiishi hilo, basi si wafuasi wa Yesu.








All the contents on this site are copyrighted ©.