Kikundi cha Boko Haram kinaendelea kusababisha maafa makubwa
Kampeni ya Serikali ya Nigeria dhidi ya Kikundi cha Kigaidi cha Boko Haram bado haijafua
dafu kwani kila siku, Kaskazini mwa Nigeria kuna watu wasiokuwa na hatia wanaoendelea
kupoteza maisha yao kutokana na mashambulizi haya. Mashambulizi yaliyofanya hivi karibuni
mji Mafa yamesababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao. Baadhi ya wananchi walilazimika
kukimbilia nchini Cameron kwa kuhofia usalama wa maisha yao.
Taarifa zinaonesha
kwamba, Boko Haram inaendelea kufanya mashambulizi pia nchini Camerun, hali ambayo
inasababisha wasi wasi mkubwa kwa wananchi walioko Kaskazini mwa Nigeria. Hali hii
itasababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao.
Umoja wa Mataifa unasema,
katika kipindi cha mwaka mmoja, zaidi ya watu laki tatu wamelazimika kuyakimbia makazi
yao, watu ambao kwa sasa wanategemea msaada kutoka Jumuiya ya Kimataifa.