2014-03-03 09:30:34

Maaskofu wa Uganda waafiki katazo dhidi ya ushoga


Kampala) Maaskofu Katoliki Uganda wameonyesha mshikamano wao na serikali katika sheria inayozuia ushoga, na wameridhia kuwekwa kwa adhabu kali kwa wale wanaotaka kufanya ushoga hadharani , kinyume na kanuni za jadi na mila katika taifa la Uganda
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Uganda, Mons. Yohana Mbatizaji Kauta, alitaja msimamo wa Kanisa Katoliki juu ya swala la ushoga kwa shirika la habari la CNS Februari 26, kwamba majibu yao na Kanisa ni wazi kabisa, hawaungi mkono ushoga. Lakini tangu mwanzo suala hili limejadiliwa wamekuwa wakipinga adhabu kali za kupita kiasi kwa vitendo vya ushoga kama kifo au kifungo cha maisha . Maaskofu kwa uelewa wao kwamba , hiki si kilema cha kuzaliwa nacho mtu bali ni kujiendekeza, adhabu za kifungo zinawe kutolewe lakini katika maana yakusaidia mtu aondokane na tabia hiyo mbovu katika jamii.

Maaskofu wanaamini kuwa kwa neema na maongozi mapya, mashoga wanaweza kubadilika. Maaskofu walijadili na kutoa tamko lao wakati wakiwa katika kipindi cha mafungo ya kiroho ambamo pia waliombea upatikanaji wa sheria mpya katika hali ya maridhiano na amani.

Sheria dhidi ya vitendo vya ushoga ilianza kutumika tarehe 24 Februari, baada ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda kutia saini hati ya sheria hiyo. Muswada awali ulipendekeza adhabu ya kifo kwa kosa la ushoga, lakini sasa sheria inataja au kifungo cha maisha jela kwa wanaobanika kufanya ushoga hadarani , badala ya mapendekezoya awali ya kifungo cha miaka 14 jela.

Nchi za Magharibi wafadhili na makundi ya haki za kimataifa wameiita sheria mpya kuwa matumizi mabaya ya haki za binadamu na wanaomba ifutwe.
Marekani, na mataifa mengine yanayofadhili Uganda yamesitisha misaada yake hadi sheria hiyo itakayofutwa, Katibu wa Nchi wa Marekani John Kerry ameeleza katika taarifa yake.








All the contents on this site are copyrighted ©.