2014-03-01 08:40:40

Kongamano la kimataifa kuhusu haki msingi za binadamu


Kanisa na Haki Msingi za Binadamu ndiyo kauli mbiu inayoongoza Kongamano la Kimataifa lililoandaliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Jamhuri ya Watu wa Slovakia hapo tarehe 4 Machi 2014. Kardinali Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa la haki na amani anatarajiwa kushiriki katika kongamano hili kwa kupembua kwa kina na mapana kuhusu: haki msingi, utu na heshima ya binadamu mintarafu Mafundisho ya Kanisa Katoliki.

Baraza la Kipapa la haki na amani linasema kwamba, lengo la Kongamano hili ni kuhamasisha ushiriki wa Kanisa mahalia katika mchakato wa kulinda na kutetea haki msingi, utu na heshima ya binadamu. Kongamano hili linawashirikisha viongozi wa Kanisa na Serikali kutoka Slovakia. Wajumbe watapata fursa ya kusikia kuhusu nyanyaso na madhulumu dhidi ya Wakristo Barani Ulaya.

Wajumbe watagusia pia haki za mashoga pamoja na uhuru wa kidini nchini Slovakia; hali halisi na changamoto zilizopoto.







All the contents on this site are copyrighted ©.