2014-02-26 14:53:27

Makumi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Yobe waua- Nigeria


Msemaji wa Tume maalum ya kijeshi katika mji wa Yobe, Kaskazini mwa Nigeria , amethibitisha uwepo wa shambulio la kighaidi, lililoua wanafunzi 29 wa Shule ya Sekondari ya Buni Yadi, Yobe, Kaskazini mwa Nigeria, usiku wa manane, Jumatatu kuamkia Jumanne, wakati wanafunzi hao wakiwa wamelala katika mabweni yao.


Msemaji wa Tume ya Kijeshi katika eneo hilo, Lazaro Eli , Jumanne alithibitisha habari hizo, bila ya kutaja idadi ya majeruhi, kwamba watu wasiojulikana, wanaodhaniwa kuwa wana kikundi wa Boko Haram,walifungulia risasi za moto kwa hosteli ya wanafunzi ya Yobe. saa nane za usiku kuamkia Jumanne.

Boko Haram wanatuhumiwa pia Septemba mwaka jana, katika mkoa huo, kufanya shambulio la kighaidi lililo ua wanafunzi 40 katika Chuo cha Kilimo cha Gujba .
Pia , mapema mwezi Julai mwaka jana , Boko Haram, walifanya mashambulizi kwa wanafunzi wa Sekondari ya Serikali , Mumoda , na kuua zaidi ya 40 ya wanafunzi.


Kw aajili ya kukabiliana na mashambulizi hayo, serikali ya Rais Jonathan imepeleka kikosi kingine cha maaskari kuongoeza nguvu ya lindo na msako wa kuwakamata waharifu .

Wanamgambo wa Boko Haram wanadai kufanya mashambulio hayo kwa kutaka eneo la Kaskazini , litawaliwe kwa sharia kali za Kiislamu, na hawataki elimu toka mataifa ya Magharibi . Na hivyo Mikoa ya Kaskazini Borno na Adamawa inayo kaliwa na Waislamu wengi zaidi imeathiriwa kwa kiwango kikubwa.

Kwa ajili ya kudhibiti utendaji wa kikundi hicho, serikali, imeliweka eneo chini ya utawala wa kidharura tangu Mei mwaka 2013 baada ya kutokea mashambulio mfululizo. Pamoja na uwepo wa utawala huo wa kidharura , bado watu wanaendelea kuuawa katika mashambulizi tofauti tofauti katika eneo hilo la Kaskazini mwa Nigeria.








All the contents on this site are copyrighted ©.