Makumi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Yobe waua- Nigeria
Msemaji wa Tume maalum ya kijeshi katika mji wa Yobe, Kaskazini mwa Nigeria , amethibitisha
uwepo wa shambulio la kighaidi, lililoua wanafunzi 29 wa Shule ya Sekondari ya Buni
Yadi, Yobe, Kaskazini mwa Nigeria, usiku wa manane, Jumatatu kuamkia Jumanne, wakati
wanafunzi hao wakiwa wamelala katika mabweni yao.
Msemaji wa Tume ya Kijeshi
katika eneo hilo, Lazaro Eli , Jumanne alithibitisha habari hizo, bila ya kutaja
idadi ya majeruhi, kwamba watu wasiojulikana, wanaodhaniwa kuwa wana kikundi wa Boko
Haram,walifungulia risasi za moto kwa hosteli ya wanafunzi ya Yobe. saa nane za
usiku kuamkia Jumanne.
Boko Haram wanatuhumiwa pia Septemba mwaka jana, katika
mkoa huo, kufanya shambulio la kighaidi lililo ua wanafunzi 40 katika Chuo cha Kilimo
cha Gujba . Pia , mapema mwezi Julai mwaka jana , Boko Haram, walifanya mashambulizi
kwa wanafunzi wa Sekondari ya Serikali , Mumoda , na kuua zaidi ya 40 ya wanafunzi.
Kw
aajili ya kukabiliana na mashambulizi hayo, serikali ya Rais Jonathan imepeleka kikosi
kingine cha maaskari kuongoeza nguvu ya lindo na msako wa kuwakamata waharifu .
Wanamgambo
wa Boko Haram wanadai kufanya mashambulio hayo kwa kutaka eneo la Kaskazini , litawaliwe
kwa sharia kali za Kiislamu, na hawataki elimu toka mataifa ya Magharibi . Na hivyo
Mikoa ya Kaskazini Borno na Adamawa inayo kaliwa na Waislamu wengi zaidi imeathiriwa
kwa kiwango kikubwa.
Kwa ajili ya kudhibiti utendaji wa kikundi hicho, serikali,
imeliweka eneo chini ya utawala wa kidharura tangu Mei mwaka 2013 baada ya kutokea
mashambulio mfululizo. Pamoja na uwepo wa utawala huo wa kidharura , bado watu wanaendelea
kuuawa katika mashambulizi tofauti tofauti katika eneo hilo la Kaskazini mwa Nigeria.