2014-02-25 11:22:24

Changamoto ya maisha na utume wa Papa Francisko kwa Kanisa la Amerika ya Kusini!


Tume ya Kipapa ya Amerika ya Kusini, tarehe 25 Februari 2014, imeanza mkutano wake wa Mwaka utakaohitimishwa hapo tarehe 28 Februari 2014 kwa kukutana na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko.

Mkutano huu unajadili pamoja na mambo mengine umuhimu wa Utume wa Papa Francisko kwa Kanisa la Amerika ya Kusini; hali ya maisha ya vijana kutoka Amerika ya Kusini; uhusiano kati ya Vijana wa kizazi kipya na wanasiasa pamoja na dhamana ya Kanisa katika malezi ya vijana wa kizazi kipya kwa kukazia haki na amani. Wajumbe pia watapembua kwa kina na mapana Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013 nchini Brazil.







All the contents on this site are copyrighted ©.