Ujumbe mzito umewasindikiza Makardinali wapya mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Sala ya Malaika wa Bwana, Jumapili tarehe 23
Februari 2014 aliwashukuru wajumbe kutoka sehemu mbali mbali za dunia walioshiriki
katika Ibada ya kuwasimika Makardinali wapya, jumamosi iliyopita pamoja na kuhudhuriwa
Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.
Baadhi
ya nchi kama Haiti na Brazil ziliwakilishwa na Marais wake. Ujumbe wa Burkina Faso
uliongozwa na Waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa; Ujumbe wa
Canada uliongozwa na Waziri wa miundo mbinu. Kimsingi, nchi zilizotuma uwakilishi
mzito ni pamoja na: Chile, Nicaragua, Ujerumani, Argentina, Corea, Jamhuri ya Wananchi
wa Visiwa vya Dominican, Vietnam, Pwani ya Pembe, Hispania, Malta pamoja na Italia.