2014-02-23 14:11:17

Papa awahimiza viongozi wa kanisa kudumisha matumaini kwa watu wa Mungu


Jumapili 23 Februari, majira ya asubuhi , katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, Papa Francisko aliongoza maadhimisho ya Ibada ya Misa akiwa na Makardinali wapya na Makardinali wengine , kwa mujibu wa liturujia ya Jumapili ya V11 katika Kipindi cha kawaida. Ibada iliyo hudhuriwa na maefu ya waamini waliofika kuwapongeza Makardinali wapya toka sehemu mbalimbalimbali za dunia.

Katika homilia yake, Papa Francisko, aliitafakari sala ya utangulizi ya Ibada :“ Baba Mwenye Huruma , kwa msaada wako , daima tuwe makini kuisikia sauti ya Roho Mtakatifu" .

Papa alisema, Sala hii ya ufunguzi wa Misa, inatukumbusha jambo msingi kwamba, ni wito wa kumsikiliza Roho Mtakatifu ambaye hulichagamsha na kuliongoza Kanisa. Kwa nguvu yake ya ubunifu na upya , Roho Mtakatifu daima hudumisha matumaini ya Watu wa Mungu, wanapo fanya hija katika njia ya historia yao , na kama Msaidizi , yeye daima huwaimarisha Wakristu katika kuwa mashaidi imara wa imani yao.

Papa alieleza na kusema wakati huo akiwa pamoja na Makardinali Wapya, ulikuwa ni wakati wa kusikiliza sauti ya Roho Mtakatifu anaye ongea nao kwa njia ya maandiko Matakatifu yaliyosomwa.

Papa baada ya kuyatafakari masomo , aliwakumbusha Makardinali kwamba, Bwana Yesu na Mama Kanisa, wanatoa mwaliko kwao, kushuhudia kwa bidii na hamasa zaidi katika nji hizi za utakatifu . Ni hasa katika zawadi hii kubwa ya majitolea binafsi, yanayotolewa kwa uhuru kamili, ambamo mna utakatifu wa kuwa Kardinali . Na kwamba kwa hadhi hii, wanapaswa kumpenda kila mmoja, hata wale wanaonekana kuwa maadui kwao, wanaolenga kuwafanyia mabaya , kuwapinga au kuwakaidi, wote ni kuwaslimia kwa tabasamu nzuri linalotokana ndani ya moyo wa msamaha,huruma na upendo wa kweli, hata kwa wale wanao fikiri hawastahili. Ni hatua ya kupinga kiburi kwa upole ; ni kuwa watu wa kusahau madharirisho na unyanyasaji wanaoweza kukumbana nao. Daima ni kuruhusu kuongozwa na Roho wa Kristo, aliye jitoa sadaka mwenyewe juu ya Msalaba, ili waweze kuwa njia kwa wengine pia , katika kuupata upendo wake, na kuwa miongozi mwa wafuasi wake.

Papa ameitaja hii kuwa ndiyo tabia ya Kardinali, ndiyo utendaji wa Kardinali. Kuitwa Kardinali katika Kanisa la Roma la Ulimwengu , si kuingia katika mahakama ya kifalme, lakini ni kujiunga katika huduma ya kina ya kusaidia wengine ili waepuke tabia mbovu na utendaji usiofaa unaochochewa na fitina, uvumi, magenge ya uovu upendeleo au kupendelewa.

Papa alieleza na kuomba lugha ya Makardinali na iwe lugha ya Injili, kusema ndiyo wakimaanisha kweli ndiyo , na hapana iwe na maana ya kweli ya hapana , na miendo na fikira zao iwe katika mtazamo wa Heri Takatifu kuwa njia yao utakatifu.
Papa alikamilisha hotuba yake kwa kuwasihi Makardinali wote kuwa wamoja katika Kristo na kati yao wenyewe kwa wenyewe. Na aliwaomba wasimsahau katika sala zao , na pia ushauri na wamsaada wao wa karibu katika kuliongoza Kansia la Ulimwengu. Vivyo hivyo alitoa mwaliko huo kwa Maaskofu, Mapadre , Mashemasi, watawa wake kwa wanaume, na walei, akisihi kuisihi pamoja na Roho Mtakatifu, na dekania ya Makardinali iweza daima kuwa na hamu zaidi na hamu ya upendo wa kichungaji uliojaa utakatifu, kwa ajili ya kutumikia Injili na kulisadia Kanisa kutoa miali ya mwanga wa Upendo wa Kristu katika dunia yetu.







All the contents on this site are copyrighted ©.