2014-02-21 09:40:02

Waziri mkuu mstaafu wa Italia anamshukuru Papa Francisko


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano jioni tarehe 19 Februari 2014 alifanya mazungumzo ya faragha na aliyekuwa Waziri mkuu wa Italia Bwana Enrico Letta. Taarifa kutoka Ikulu ya Italia inasema kwamba, mazungumzo haya yalikuwa ni ya maana sana.

Waziri mkuu mstaafu Letta ameguswa sana na mazungumzo yake na Baba Mtakatifu Francisko na amemshukuru na kwamba, ataendelea kutunza moyoni mwake mazungumzo haya hata kwa siku za usoni! Bwana Letta ambaye anatoka Chama tawala cha PD, tarehe 14 Februari 2014 aliamua kung'atuka kutoka madarakani baada ya kushambuliwa na Chama chake kutokana na kusua sua kufanya mabadiliko makubwa katika masuala ya kiuchumi. Matteo Renzi ndiye aliyepewa dhamana ya kuunda Serikali Mpya ya Italia kwa sasa.







All the contents on this site are copyrighted ©.