2014-02-18 15:32:09

Vishawishi vya majaribu huweza kuua, lakini Neno la Yesu huokoa.


(Vatican) Kushinda upotofu wa vishawishi vya majaribu inawezekana tu kwa kusikiliza Neno la Yesu. Papa Francisko alieleza katika homilia yake wakati wa Ibada ya Misa ya Jumanne asubuhi, aliyo iongoza katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta mjini Vatican. Alisema pamoja na udhaifu wetu , daima Kristo hutupatia imani na kufungua upeo wa macho na uwezo, katika kuiona mipaka yetu.

Majaribu huonekana kama kivutio poa ambacho taratibu humwingiza mtu dani ya ngome na kumfanya kuwa mtumwa na kiziwi kwa neno la Mungu. Hotuba ya Papa Francisko ilieleza ukweli huo kufanya rejea mfululizo wa maelezo ya Mtakatifu Yakobo, kama ilivyokuwa katika somo la Liturujia. Papa alieleza Ukweli kwamba Mungu hamtengi binadamu yoyote, ila binadamu hujitenga mwenyewe kwa nia na tamaa zake mbaya . Mtume Yakobo anasema, tamaa huzalisha dhambi. Na dhambi huzalisha mauti.

Papa aliendelea kuuliza majaribu hutoka wapi ? Na kwa jinsi gani hututendea ndani mwetu ? alisema ,maelezo ya Mtume Yakobo, yanatuambia kwamba, majaribu hayatoki kwa Mungu , lakini hutokana na tamaa zetu, udhaifu wetu wa ndani, ambao ni kovu la majeraha ya dhambi ya asili, ambalo likiendekezwa huzaa majaribu kutokana na tamaa hizo.
Na kwamba majaribu yana sifa tatu, ni kujiimarisha na kujionyesha na kuvutia. Papa anasema, hujiimarisha na kutoa kishawishi kama ni haki. Na hufanyika katika hali ya kuvutia na utulivu, kama Yesu mwenyewe alivyo eleza katika mfano wa ngano na magugu. Ngano ina magugu yaliyopandwa na adui vilikua pamoja. Hivyo majaribu hukua ama hakuna cha kuyazuia.

Papa aliendela kuasa kwamba, hivyo , wakati wa majaribu, tunakatishwa hamu ya kuisikiliza sauti ya Mungu, tunakataa kusikiliza neno lake. Tunazongwa na kushindwa tunakuwa hatuelewi. Na Yesu alikumbusha wakati wa muujiza wa kuzidisha mikate, aliwaambia watoke nje ya mazingira ambayo , yalikuwa yamefunga mioyo yao na upeo wa akili na macho yao na hivyo wakiongozwa katika kutenda dhambi. Hivyo kusikiliza tu Neno la Mungu, Neno la Yesu la kuokoa. Kusikia Neno la Mungu ni kufungua upeo wa macho ... Yeye daima hutufundisha jinsi ya kuepuka majaribu. Yesu ni Mkuu , kwa sababu, si tu hutuwezesha kuyashinda majaribu , lakini pia hutupatia uwezo a kujiamini zaidi katika kukataa vishawishi vya majaribu.

Imani hii , Papa anasema, ina nguvu kubwa. Na wakati wa kujaribiwa Bwana anatarajia, imani yetu kuwa imara kuishinda dhambi. Daima ni kufungua upeo wa akili na macho, kukataa kwa kuwa kinyume chake, mara kwa mara, ni kuelekea kuzimu. Majaribu huja kama ilivyokuwa wakati wa mashua ya Mitume ilipopigwa na upepo. Kwenye mazingira ya namna hii, alimalizia Papa , inawezekana tu kushinda majaribu kwa kusikiliza neno la Yesu .

Hivyo , "Tunaomba kwa Bwana siku zote , kama walivyofanya Mitume, na kwa uvumilivu wake , wakati sisi tunapambana na majaribu, Yeye awe karibu nasi kutuhimiza tusikubali kushindwa au kuwa na wasiwasi,lakini tuyakumbuke mengi aliyo tututendea kwa neema zake wakati ule. Bwana anasema, inua macho yako na utazame upeo wa macho, si karibu, bali ni kusonga mbele. Ni hili Neno la kuokoa wakati wa kuaguka katika dhambi na wakati wa majaribu".








All the contents on this site are copyrighted ©.