Vita, kinzani na migogoro inayoendelea kujitokeza Barani Afrika imekuwa ni chanzo
kikubwa cha taabu na mahangaiko ya watu wasiokuwa na hatia. Kuna watu wanalazimika
kuyakimbia makazi yao, wanateseka kwa njaa na magonjwa kutokana na ukosefu wa amani
na utulivu.
Baba Mtakatifu Francisko kwa kuguswa na mahangaiko ya wananchi
wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, anawaalika watumiaji wa mitandao ya kijamii, kumuunga
mkono katika kusali kwa ajili ya kuombea amani na utulivu huko Jamhuri ya Watu wa
Afrika ya Kati na Sudan ya Kusini.