Mshikamano wa dhati na wasichana wanaoishi kwenye mazingira hatarishi
Kikundi cha wake wa Viongozi (Millenium Women Group) kimetoa msaada wa Chakula, Mavazi
na Vifaa vya usafi vyenye thamani ya sh. Milioni 6.8/- kwa “New Hope for Girls Organization’’
kinacholea wasichana wanaoishi katika mazingira magumu.
Mke wa Waziri Mkuu
Mama Tunu Pinda alieleza kuwa, wake wa viongozi waliguswa baada ya kukutana na Bibi.
Consoler Eliya mwaka jana katika mkutano wa wanawake wajiwezeshe kiuchumi ambaye ni
miongoni mwa wasichana walioishi katika mazingira magumu na kuahidi kumsaidia.
Misaada
hiyo ilitolewa kwenye makazi ya Waziri Mkuu Oysterbay, jijini Dar es Salaam “Akina
mama wameona jitihada za Bibi. Consoler katika kusaidia wasichana hawa wanaoishi katika
mazingira magumu, ambayo watu wengi wamekuwa wakiyapitia na kushindwa kujitolea kama
ilivyokuwa kwa Bibi. Consoler’’,alisema.
Mama Pinda aliongezea kuwa, nia ya
Serikali ni kuhakikisha watoto husasani wakike wanaishi kwa amani na kupata haki zao
za msingi kwani maisha yao yamekuwa ya huzuni kubwa mno.
Baada ya makabidhiano
hayo, Bibi Consoler Eliya, aliwashukuru sana wake wa viongozi kwa msaada waliotoa:
“mhitaji si lazima awe yatima, mhitaji anaweza kuwa na wazazi wote na bado akawa anaishi
katika mazingira magumu hivyo sisi tunaishi na watoto walitoka katika makundi tofauti
ya mazingira magumu’’ alisema. Mbali na kulelewa katika kituo hicho, pia wasichana
hao wanabuni na kutengeneza vitu kama batiki, mikufo ambayo inasaidia kuendesha maisha
yao, aliongezea Bibi. Consoler.
Mwenyekiti wa kikundi hicho Mama Lukuvi aliongezea
kuwa, kutokana na juhudi zinazooneshwa na wasichana hao Kikundi kitawawezesha meza
katika mkutano wa wajasiriamali utakaofanyika hivi karibu Jijini Dar es Salaam ili
waweze kupeleka bidhaa zao za ubunifu wanazozitengeneza.