Mshikamano wa kidugu kwa watu walioguswa na ajali ya moto mjini Buenos Aires, Argentina!
Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam na rambirambi kwa wale wote waliokumbwa na
ajali ya moto iliyotokea siku ya Jumatano tarehe 5 Februari 2014, huko Buenos Aires
nchini Argentina. Watu tisa wamepoteza maisha, wengine saba wamejeruhiwa na watu kadhaa
walikuwa hawajulikani mahali walipo! Serikali ya Argentina imetangaza siku mbili za
maombolezo ya kitaifa.
Baba Mtakatifu katika ujumbe wake aliomwandikia Askofu
mkuu Mario Aurelio wa Jimbo kuu la Buenos Aires anaonesha masikitiko yake makuu kwa
maafa haya makubwa yaliyowapata wananchi wa Argentina. Anaendelea kuungana nao katika
sala na sadaka yake, ili Mwenyezi Mungu mwingi wa huruma na mapendo, aweze kuwafariji
wote waliofikwa kwa msiba huu.
Anawaalika wananchi wa Argentina kuonesha moyo,
mshikamano na upendo wa kidugu kwa wote walioguswa na maafa haya, anawafariji wote
na kuwapatia baraka zake za kitume!