2014-02-06 08:56:07

Vatican itatekeleza maoni yaliyotolewa, lakini haitakubali kuingiliwa katika Mafundisho tanzu ya Kanisa!


Baada ya kumalizika kwa mkutano wa sitini na tano wa kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Mtoto na kutoa maoni yake baada ya kujadili kwa kina na mapana taarifa iliyowasilishwa kwenye mkutano huu na ujumbe wa Vatican pamoja na nchi nyingine wanachama yaani Congo, Ujerumani, Ureno, Russia na Yemen.

Kadiri ya mchakato ulioainishwa kwenye mkataba wa Haki za Mtoto, Vatican itaendelea kuyafanyia kazi maoni yaliyotolewa kuhusu taarifa yake kwa kuheshimu haki na utekelezaji wake kimataifa bila kusahau mchango wa Vatican wakati wa mkutano huo uliofanyika hapo tarehe 16 Januari 2014.

Vatican inasikitika kuona kwamba, baadhi ya maoni yaliyotolewa na kamati hii yana mwelekeo wa kutaka kuingilia na kuvuruga Mafundisho Tanzu ya Kanisa Katoliki kuhusu utu na heshima ya binadamu pamoja na utekelezaji wake wa uhuru wa kidini. Vatican inaendelea kujikita katika kulinda na kutetea haki msingi za watoto mintarafu kanuni na njia zilizoainishwa kwenye Mkataba wa Haki za Mtoto pamoja na kuzingatia tunu msingi za maisha ya kimaadili na kiroho zinazofundishwa na Kanisa Katoliki.







All the contents on this site are copyrighted ©.