2014-02-06 09:16:25

Kesi ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 yaanza kusikilizwa nchini Ufaransa, baada ya miaka 20!


Baada ya kuyoyoma miaka ishirini tangu yaliyopotokea mauaji ya kimbari nchini Rwanda kunako Mwaka 1994 na kusababisha watu 800, 000 kupoteza maisha, mapema juma hili, kesi ya mauaji ya kimbari imeanza kusikilizwa mjini Paris, Ufaransa.

Kwa takribani miaka ishirini uhusiano kati ya Rwanda na Ufaransa ulisuasua kwa kiasi kikubwa, lakini kwa sasa inaonekana kana kwamba, historia inazidi kusonga mbele. Hayo yamesemwa na Johnston Businge, Waziri wa sheria nchini Rwanda na kwa upande wake, Laurent Fabius anasema ni vyema ikiwa kama kesi hii imepata mahali pa kusikilizwa.

Kwa miaka kadhaa Serikali ya Rwanda ilikuwa inawadaia watuhumiwa wa mauaji ya kimbari waliokuwa wamekimbilia nchini Ufaransa kurudishwa nchini Rwanda ili kujibu shutuma za mauaji ya kimbari zilizokuwa zinawakabili, lakini kwa miaka hii yote Serikali ya Ufaransa ilikataa kuridhia ombi la Serikali ya Rwanda.







All the contents on this site are copyrighted ©.