Rais Tui Atua Tamasese Efi akutana na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko siku ya Jumatatu, tarehe 3 Februari 2014 amekutana na kuzungumza
na Rais Tui Atua Tupua Tamasese Efi wa Visiwa vya Samoa, ambaye baadaye alikutana
na kuzungumza na Askofu mkuu Pitero Parolin, katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana
na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano
wa kimataifa mjini Vatican.
Katika mazungumzo ya viongozi hawa wawili, wamejikita
katika hali ya uchumi na kisiasa pamoja na kuangalia mchango wa Kanisa Katoliki katika
mchakato wa maendeleo na ustawi wa wananchi wa Samoa katika medani mbali mbali za
maisha. Wamebadilishana mawazo kuhusu masuala ya kimataifa hasa umuhimu wa ushirikiano
wa Kikanda, utunzaji bora wa mazingira katika nchi zilizoko kwenye Bahari ya Pacific.