Mheshimiwa Padre Vincent Mduduzi Zungu ateuliwa kuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki Port
Elizabeth, Afrika ya Kusini
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Mheshimiwa sana Padre Vincent Mduduzi Zungu, kutoka
Shirika la Ndugu Wafrancisko Wakapuchini kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Port
Elizabeth, Afrika ya Kusini. Kabla ya uteuzi huu Askofu mteule alikuwa ni msimamizi
Wakapuchini kutoka Kusini mwa Afrika, kwenye Makao Makuu ya Shirika mjini Roma.
Askofu
mteule Vincent Mduduzi Zungu alizaliwa tarehe 28 Aprili 1966, Jimboni Eshowe. Baada
ya majiundo na malezi ya Kipadre na kitawa, akaweka nadhiri zake za daima hapo tarehe
2 Julai 1994 na kupewa Daraja Takatifu la Upadre tarehe 8 Julai 1995.
Baada
ya Upadrisho alitekeleza utume wake kama Paroko msaidizi, Mlezi wa Wanovisi, Jalim
na baadaye alichaguliwa kuwa ni Padre Mkuu wa Kanda ya Wakapuchini Afrika ya Kusini.
Itakumbukwa
kwamba, tangu Mwaka 2011 Jimbo la Port Elizabeth lilikuwa wazi baada ya Askofu Michael
Gower Coleman kung'atuka kutoka madarakani kwa sababu za kiafya.