Si habari kumsifia Papa Francisko na kumtupia "madongo" Benedikto XVI!
Padre Federico Lombardi msemaji mkuu wa Vatican anabainisha kwamba, Baba Mtakatifu
Francisko anaendelea kuwa na mvuto mkubwa kwa vyombo mbali mbali vya upashanaji habari.
Wengi wanachambua mambo mazuri yanayofanywa na Baba Mtakatifu Francisko katika kulinda
na kuwatetea wanyonge na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii.
Hili ni
jambo jema kama ambavyo Jarida la "Rolling Stone" lilivyoandika na habari zake kusambaa
kama umande wa asubuhi. Padre Lombardi anasema, inasikitisha kuona kwamba, Jarida
hili linaandika mambo mazuri ya Papa Francisko wakati huo huo linamtupia "madongo"
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI.
Huu si uandishi wa habari wenye tija
wala mashiko kwa Papa Francisko anayetambua na kuthamini mchango mkubwa uliofanywa
na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI katika maisha na utume wa Kanisa!