Mshikamano wa Papa Francisko na wahanga wa ajali ya moto nchini Canada!
Baba Mtakatifu Francisko hivi karibuni alituma salam za rambi rambi kwa Askofu mkuu
Pierre-Andrè Fournier wa Jimbo kuu la Rimouski, Canada kutokana na ajali ya moto uliounguza
makazi ya wazee huko Lisle Verte na hivyo kusababisha watu 32 kupoteza maisha, wengine
wengi kujeruhiwa na wengi hadi sasa hawajulikani waliko.
Ujumbe wa Baba Mtakatifu
umeandikwa kwa niaba yake na Kardinali mteule Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican
na kwamba, Baba Mtakatifu yuko karibu na wote waliofikwa na msiba huu kwa njia ya
sala. Anapenda kuwazamisha wote waliofariki dunia katika huruma ya Mungu ili waweze
kuina nuru ya uzima wa milele. Baba Mtakatifu anapenda kuzifariji familia na wote
waliopata majeraha na kwamba, anawaombea ili waweze kupona haraka.
Baba Mtakatifu
anakipongeza kikosi cha zimamoto kwa kazi kubwa kilichofanya katika jitihada za kuokoa
maisha ya watu na mali zao. Wote hawa anawapatia baraka zake za kitume!