2014-01-30 08:29:28

Bravo! Padre Federico Lombardi, SJ!


Tume ya Mawasiliano ya Jamii, Baraza la Maaskofu Katoliki Hispani, tarehe 5 Februari 2014 itatoa tuzo maalum kwa wanahabari waliotukuka katika utume wao kwenye uringo wa bahari kwa Mwaka 2013.

Lengo la tuzo hii ya hali ya juu kutolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Hispania inalenga kutambua mchango unaotolewa na wanahabari katika medani mbali mbali za maisha, kwa kujipambanua zaidi kwa kusimama kidete kulinda na kutetea utu na heshima ya binadamu; haki msingi za binadamu sanjari na tunu msingi za Kiinjili.

Kwa mwaka 2013, tuzo hii anapewa Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican ambaye pia ni Mkurugenzi mkuu wa Radio Vatican. Itakumbukwa kwamba, miezi michache iliyopita alikuwa pia ni mkurugenzi mkuu wa Kituo cha Televisheni cha Vatican. Huu ni utume unaohitaji mtu kujisadaka ili kutekeleza majukumu yote haya kwa juhudi, maarifa, bidii na weledi.

Waswahili wanasema, kwa Padre Lombardi, "hapa upele ulipata mkunaji!". Ni kiongozi asiyependa makuu, lakini mwaminifu na mchakapakazi.

Baraza la Maaskofu Katoliki Hispania pia litatoa tuzo kwa Kampuni ya "Algencia 101" inayosimamia na kuratibu akaunti ya Baba Mtakatifu Francisko @Pontifex. Kampuni hii imepewa tuzo huu kwa kucharuka katika matumizi ya teknolojia mpya ya njia za mawasiliano ya jamii.







All the contents on this site are copyrighted ©.