Baba Mtakatifu Francisko amekubali ombi lililowasilishwa kwake na Askofu Michele Russo
wa Jimbo Katoliki Doba la kutaka kung'atuka kutoka madarakani kadiri ya sheria za
Kanisa namba 401, Ibara ya 2.
Wakati huo huo, Baba Mtakatifu amemteua Askofu
Miguel Angel Sebastian Martinez, M.C.C.J wa Jimbo la Lai, Chad kuwa Msimamizi wa kitume
wa Jimbo Katoliki Doba.