2014-01-29 10:08:01

Itawagharimu sana wananchi wa Sudan ya Kusini kuanza ujenzi wa miundo mbinu iliyoharibiwa kutokana na vita!


Miundo mbinu ya Jimbo Katoliki la Malaka, Sudan ya Kusini imeharibiwa vibaya kutokana na vita iliyopamba moto kwa takribani mwezi mmoja uliopita. Ujenzi wa miundo mbinu hii ulifanywa kwa kipindi cha miaka minane ya shida na sadaka kubwa kutoka kwa waamini, wafadhili na watu wenye mapenzi mema, lakini kufumba na kufumbua kila kitu kimebaki kuwa ni majivu. Haya ndiyo madhara ya vita inayoshabikiwa na watu wanatafuta madaraka kwa nguvu bila kuangalia masilahi na mafao ya wengi!

Hayo yamesemwa jumapili iliyopita, tarehe 26 Januari 2014 na Monsinyo Roko Taban Musa, Msimamizi wa kitume wa Jimbo Katoliki la Malakal, wakati wa Maadhimisho ya Ibada ya Misa Takatifu kwenye Parokia ya Mtakatifu Kizito, Jimbo kuu la Juba.

Maeneo yaliyoharibiwa vibaya na vita Sudan ya Kusini ni pamoja na Upper Nile, Unità pamoja na Jonglei. Itawagharimu sana wananchi wa Sudan ya Kusini kuweza kurejesha amani na utulivu kwani hadi sasa Serikali na Wapinzani wanarushiana "madongo" kwa kuvunja mkataba wa kusitisha vita uliotiwa sahihi hivi karibuni.







All the contents on this site are copyrighted ©.