Wakristo wanaendelea kuhamasishwa kusali kwa ajili ya umoja wa Wakristo kwani utengano
bado ni kashfa kubwa inayozuia ushuhuda wa pamoja miongoni mwa Wakristo katika mchakato
wa utangazaji wa Habari Njema ya Wokovu.
Hivi karibuni, Wakristo wamefunga
juma la kuombea Umoja wa Wakristo, tafakari kwa Mwaka huu iliandaliwa na Wakristo
kutoka Canada kwa kuongozwa na kauli mbiu "Je, Kristo amegawanyika!"
Baba Mtakatifu
Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anawaalika waamini
kusali kwa ajili ya kuombea Umoja wa Wakristo. Kuna mambo msingi yanayowaunganisha
Wakristo! Ubatizo na Msalaba wa Kristo!