Papa kuadhimisha Siku ya Watawa Duniani, Jumapili 2 Februari 2014 mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko katika Maadhimisho ya Siku kuu ya Kutolewa Bwana Hekaluni
sanjari na Siku ya Watawa Duniani, Jumapili ijayo tarehe 2 Februari 2014, kuanzia
saa 4:00 asubuhi kwa saa za Ulaya anatarajiwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye
Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.
Tiketi za kuingilia kwenye Ibada
hii zinapatikana kwenye Ofisi za Baraza la Kipapa la Mashirika ya Kitawa na Kazi za
Kitume iliyoko mjini Roma kuanzia Alhamisi tarehe 30 hadi Ijumaa tarehe 31 Januari
2014, kuanzia saa 2:30 hadi saa 7: 00 Mchana.