2014-01-27 09:24:30

Vijana Wakatoliki Italia wachangia ujenzi wa Kituo cha michezo kwa watoto nchini Haiti


Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Sala ya Malaika wa Bwana aliwasalimia vijana 3000 wa Chama cha Vijana Wakatoliki Italia, waliofanya maandamano makubwa, wakiwa pamoja na wazazi na walezi wao kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, jumapili iliyopita, tarehe 26 Januari 2014. Haya ni maandamano ya amani yaliyoongozwa na kauli mbiu "hakuna mchezo bila ya uwepo wako".

Katika ujumbe wao, vijana hawa wamemwambia Baba Mtakatifu Francisko kwamba, licha ya mapungufu na karama zao, bado wanapendwa na kuthaminiwa na Mwenyezi Mungu, kiasi kwamba, wako tayari kushiriki katika furaha na upendo wa Mungu wanaonjeshana wakati wanapokuwa michezoni.

Lakini, si mahali pote kwamba, furaha na upendo huu unaweza kujionesha katika ndiyo maana katika kujinyima kwao wamekusanya kiasi cha fedha kitakachotumika katika ujenzi wa kituo cha michezo kwa ajili ya watoto wa Haiti ili kuwajengea tena matumaini na furaha ya mshikamano wa kidugu.

Watoto hao wawili mvulana na msichana kwa pamoja walirusha njiwa kama mjumbe wa amani kwa watu wa mataifa, lakini kwa watu wenye kiu ya amani duniani. Vijana hawa wamemshukuru na kumpongeza Baba Mtakatifu Francisko kwa unyenyekevu unaojionesha katika maisha na utume wake.







All the contents on this site are copyrighted ©.