Kwa kawaida binadamu ni mwepesi mno kupiga magoti kumlilia na kumwomba Mwenyezi Mungu
katika shida na mahangaiko yake ya ndani. Hili ni jambo linalofanywa na wengi. Baba
Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema,
Je, waamini watajifunza lini kurudi na kumshukuru na kumwabudu Mwenyezi Mungu kwa
ukarimu na wema anaoendelea kuwatendea waja wake?
Wataalam wanasema, Falsafa
ya Neno asante ni kuomba tena! Waamini wajifunze kuomba, kushukuru na kumwabudu Mungu
katika roho na ukweli! Tarehe 25 Januari, Kanisa linaadhimisha Siku kuu ya Wongofu
wa Mtume Paulo, mwalimu wa Mataifa. Ni kipindi cha kumshukuru na kumwabudu Mungu kwa
wema na ukarimu wake katika mafanikio yaliyokwishakupatikana katika mchakato wa majadiliano
ya Kiekumene miongoni mwa wafuasi wa Kristo!