2014-01-25 16:17:00

Jengeni madaraja ya mazungumzo, sio kuta za chuki na fitina


Wakristo ni lazima kujenga madaraja ya mazungumzo, na sio kuta za chuki na fitina. Baba Mtakatifu Francisko alihimiza wakati wa Ibada ya Misa ya asubuhi ya Ijumaa aliyoongoza katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta, mjini Vatican. .

Papa Francisko alitafakari somo la Somo la kwanza juu ya mgogoro uliokuwepo kati ya Mfalme Sauli na Daudi, akisema kuna wakati Daudi alipata na nafasi ya kumuua Sauli, lakini, hakufanya hivyo, badala yake alichukua maamuzi ya kufuata njia ya mazungumzo, kufanya amani.

Na ndivyo inavyotakiwa kwa Wakristo wote duniani, lazima kufuata njia ya majadiliano na maafikiano kwa amani, kwa sababu Yesu alitufundisha kufanya hivyo. Wapendeni adui zenu na waoombeeni. Yeye mwenyewe Yesu akiwa msalabani aliwaombea adui zake akisema, Baba Wasamehe maana hawajui walifanyalo. Hivyo ndivyo Yesu anavyotaka tuwasamehe na kuwaombea wale wanao tuchukia. Yesu ametuonyesha njia hii, kwmaba ni kuingia katika majadiliano katika hali ya upole na unyenyekevu, licha ya mashambulizi makali. Ni muhimu , kuwa mnyenyekevu na mlaini lakini bila kukubali kupokonywa imani kwa Yesu, Bwana wa Upatanisho.

Papa alieleza huku akionyesha kutambua kwamba, ni kweli siyo rahisi kujenga hali ya mazungumzo, hasa wakati wa migawanyiko mikali ya chuki.Sote tunafahamu kuwa upole na unyenyekevu , hukimeza kiburi cha mwingine, na ni muhimu kufanya hivyo, kwa sababu, kwa njia hiyo, polepole amani na kuheshimiana huanza kujengeka .

Kujinyenyekeza pengine huwa ni vigumu , lakini Mkristu anapaswa kutambua kwamba, kuruhusu chuki kuvimba moyoni ni mbaya zaidi kuliko kuanza kujenga madaraja ya majadiliano. Kuruhusu chuki kukua, huongoza katika hali ya upweke na uchungu mkali wa uadui wenyewe. Kuwa Mkristo, hivyo maana yake ni kuwa mjenzi wa madaraja ya mazungumzano.
Ni muhimu , Papa Francisko aliendelea , kutoruhusu muda mrefu kupita baada ya dhoruba za chuki na kushambuliana kutokea. Ni vyema kujenga mazungumzo haraka iwezekanavyo , kwa ajili ya kuzuia kuta za chuki kukua ni kama vile mkulima asivyoruhusu magugu kukua katika shamba lake la nafaka. Ukuta wa chuki ukisha kuwa mkubwa , inakuwa ni kazi ngumu kuubomoa na kujenga maridhiano.
Papa alihitimisha kwa kuonyesha hofu yake katika uwepo kuta zinazojengeka kila siku, kuta za chuki na fitina za muda mrefu, akiomba Wakristu wote wafuate mfano wa Daudi , ambaye alishinda chuki kwa kitendo cha unyenyekevu. .








All the contents on this site are copyrighted ©.