2014-01-24 08:01:24

Wananchi wanaoishi diaspora wanao mchango mkubwa kwa ustawi na maendeleo ya nchi zao!


Dr. James Msekela Balozi wa Tanzania nchini Italia na mwakilishi wa Tanzania kwenye Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyoko mjini Roma, hivi karibuni ameupongeza Umoja wa Wanafunzi Wakatoliki Watanzania mjini Roma, kwa kuonesha uhai, umoja, mshikamano na demokrasia. Ni matumaini ya ubalozi wa Tanzania nchini Italia kwamba, utaendelea kuboresha ushirikiano kwa ajili ya mafao na ustawi wa watanzania na Kanisa katika ujumla wake. RealAudioMP3

Amesema, umoja na mshikamano ni mambo muhimu sana katika kukabiliana na hali mbali mbali za maisha, hasa wanapokuwa ugenini. Amewataka watanzania wanaoishi diaspora kusaidiana kwa hali na mali pamoja na kufahamiana ili kubadilisha uzoefu na mang’amuzi ya maisha.

Wananchi wanaoishi “diaspora” wana mchango mkubwa katika ustawi na maendeleo ya nchi zao, kumbe, ni changamoto kwa watanzania kuonesha moyo wa uzalendo na upendo kwa nchi yao kwa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maboresho ya maisha ya watanzania wengi.








All the contents on this site are copyrighted ©.