2014-01-24 11:58:06

Misri haikualikwa Ikulu ya Marekani wakati mkutano wa wakuu wa Nchi za Kiafrika mwezi Agosti, 2014


Serikali ya Misri imesikitishwa na kitendo cha Ikulu ya Marekani kutoialika kushiriki katika mkutano kati ya Serikali ya Marekani na Viongozi wakuu wa Serikali kutoka Barani Afrika, utakaofanyika mjini Washington DC, kati ya tehe 5 na 6 Agosti 2014. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Misri anasema, uamuzi huu si wa busara na wala hauna mtazamo mpana.

Ikulu ya Marekani imejibu shutuma hizi kwa kusema kwamba, uamuzi huu hauna sababu zozote za kisiasa.

Itakumbukwa kwamba, Misri ilisimamishwa kuwa mwanachama wa Umoja wa Afrika baada ya kumwondoa kutoka madarakani Rais Mohammed Mursi aliyekuwa amechaguliwa kidemokrasia.







All the contents on this site are copyrighted ©.