2014-01-23 15:30:21

Wivu , chuki, kijicho na uzushi huleta mgawanyiko unaoharibu umoja wa Wakristu.


Mapema Alhamis hii, ikiwa ni siku ya Sita katika Wiki Maalum ya Kuombea Umoja wa Wakristu, Baba Mtakatifu Fransicko akiongoza Ibada ya Misa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta ndani ya Vatican, ameonya kwamba, wivu, chuki na hasida, huleta migwanyiko na utengano unaoua umoja wa Wakristu.
Papa alieleza kwa kutafakari masomo ya Siku ambamo somo la kwanza, linazungumzia ushindi wa Israeli dhidi ya Wafilisti kupitia ujasiri wa kijana mdogo Daudi. Furaha ya ushindi wa Daudi, mara inayogeuka kuwa huzuni, wivu na chukizo kwa Mfalme Saulo, mbele ya wanawake waliokuwa wakimsifu Daudi kwa kumuua Goliati. Hivyo, ushindi mkubwa wa Daudi unakuwa sababu ya Mfalme Saulo, kujenga chuki dhidi ya Daudi , kama ilivyotokea pia kwa KainI, ambaye moyo wake uliliwa na mdudu wa husuda na wivu dhidi ya mafaniko ya ndugu yake Abel. Na ndivyo wivu na husuda unavyorarua pia mioyo yetu , kwa kutujaza chuki na uovu wa kutovumilia wengine, ndugu zetu wake kwa waume, wanaopata mafanikio ambayo sisi hatuna.
Papa Francisko anasema, Wivu huongoza katika mauaji. Wivu ni mlango mkuu alioingilia shetani duniani , kama Biblia inavyosema : kwa wivu wa shetani, maovu yaliingia duniani. Wivu na chuki hufungua milango yote ya mambo maovu, ikiwepo migawanyiko ya kijamii. Hata Jumuiya ya Kikristo, huweza kumwezwa na dhambi hii ya wivu na chuki na ubinafsi, unaoelekeza katika kujitenga na wengine. Papa ameiitia kuwa hii ni sumu kali, kama tunavyoona katika habari za Kain na Abel.
Papa aliendelea kumweleza mtu mwenye wivu, kuwa si mtu wa amani, ni mtu mkali asiyejua kusifu, wala maana ya furaha.Daima ni mtu wenye kutazama wengine kwa kijicho na fitina kwa nini yule anavyo na nini mimi sina. Na hii husababisha uchungu, , uchungu mkubwa unaoweza kuenezwa kwa jamii nzima. Wivu ni silaha ya shetani katika kuharibu wengine. Papa ameeleza na kurejea Injili ya Yohane inayosema, "kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji".
Na alimalizia homilia yake akisema , leo hii, na tutoleee maombi yetu kwa Bwana kwa ajili ya Jumuiya zetu za Kikristo , ili ziweze kuiong’oa mbegu hii ya wivu na kamwe isipandwe kati yetu , maana wivu hauna nafasi katika mioyo yetu, na katika moyo wa jumuiya zetu,. Ila tuweze kusonga mbele na sifa kwa Bwana. Na kumsifu Bwana kwa furaha, ni neema kubwa , neema ya kutoanguka katika huzuni na wasiwasi na upinzani unaozushwa na wivu, husuda na kijicho.










All the contents on this site are copyrighted ©.