Bi Catherine Samba-Panza achaguliwa kuongoza Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati
Wajumbe wa Baraza la Mpito nchini Jamhuri ya Watu wa Afrika ya kati, limemchagua Bi
Catherine Samba Panza, mwenye umri wa miaka 56 Meya wa Jiji la Bangui, kuwa Rais wa
Kipindi cha Mpito nchini humo. Rais mteule ambaye kitaaluma ni mwanasheria na mwanamke
wa kwanza kuongoza Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati anayo changamoto kubwa ya kuhakikisha
kwamba, anahitisha uchaguzi mkuu kabla ya mwisho mwa Mwaka 2014.
Wachunguzi
wa masuala ya kisiasa wanasema, pengine huu ni mtihani mkubwa kutokana na ukweli kwamba
majengo mengi ya Serikali yameharibiwa vibaya kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe
nchini humo iliyozuka Mwezi Machi 2013 baada ya Serikali halali kupinduliwa na Kikosi
cha Seleka. Rais mteule amewataka wanajeshi wa Seleka na Balaka kusitisha mapigano
na Jumuiya ya Kimataifa kusaidia ujenzi wa nchi utakaojikita katika ukweli, haki,
amani na upatanisho wa kitaifa.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon
amempongeza Rais Catherine Samba Panza kwa kuchaguliwa kwake na kwamba, huu ni mwanzo
wa mchakato wamabadiliko ya kweli nchini humo. Changamoto kubwa kwa sasa ni kuhakikisha
kwamba, wananchi wanapata msaada kutoka katika Jumuiya ya Kimataifa ili kukabiliana
na hali ngumu kwa sasa