2014-01-20 08:01:30

Sheria za nchi zisingatie pia utu, heshima na utamaduni wa kiafrika!


Wananchi wengi nchini Nigeria wanampongeza Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria kwa kupitisha muswada wa sheria unaopiga marufuku ndoa za watu wa jinsia moja nchini Nigeria kwani vitendo hivi ni kinyume cha utu, heshima na utamaduni wa kiafrika.

Wananchi wanampongeza Rais kwa kuonesha msimamo dhidi ya kampeni za wanaharakati wanaotaka kutumia mgongo wa demokrasia na uhuru usiokuwa na mipaka kuhalalisha matendo ambayo yanakwenda kinyume cha utu na heshima ya binadamu. Hadi sasa kuna nchi 38 Barani Afrika ambazo zinapiga rufuku ndoa za watu wa jinsia moja. Baadhi ya nchi kama vile Mauritania, Sudan Kongwe na Uganda, watuhumiwa wanapokamatwa wanaweza kupata adhabu ya kifo.

Wakati huo huo, Rais Yower Kaguta Museveni wa Uganda baada ya kupata shinikizo kutoka kwa wanaharakati na baadhi ya Nchi za Ulaya kwa kutishia kusitisha kutoa misaada kwa Uganda, Rais Museveni ameamua kuurudisha muswada wa sheria bungeni ili uweze kujadiliwa tena! Muswada wa sheria Uganda ulikuwa unataka washitakiwa watakaotiwa hatiani wapewe adhabu ya kifungo cha maisha jela.








All the contents on this site are copyrighted ©.