2014-01-20 09:05:45

Mabadiliko katika Baraza la Mawaziri Tanzania.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amepangua Baraza la Mawaziri kwa kuwatema Mawaziri 5 katika orodha mpya. Mawaziri 3 wamepandishwa cheo na wengine 10 ni sura mpya katika Baraza la Mawaziri Tanzania. Dr. Asha-Rose Migiro ameteuliwa kuwa ni Waziri wa Katiba na Sheria. Bi Saada Mkuya Salum ameteuliwa kuongoza Wizara ya Fedha.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-

1.0 OFISI YA RAIS

Hakuna mabadiliko.

2.0 OFISI YA MAKAMU WA RAIS

2.1 Waziri wa Nchi (Muungano) - Hakuna mabadiliko

2.2 Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb)
Waziri wa Nchi (Mazingira).

2.3 Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb)
Naibu Waziri


3.0 OFISI YA WAZIRI MKUU

Hakuna mabadiliko

4.0 WIZARA

4.1 WIZARA YA FEDHA

4.1.1 Mhe. Saada Mkuya SALUM (Mb)
Waziri wa Fedha
Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA (Mb)
Naibu Waziri wa Fedha
4.1.2 Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb)
Naibu Waziri wa Fedha


4.2 WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Hakuna mabadiliko


4.3 WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

4.3.1 Mhe. Dkt. Asha-Rose Mtengeti MIGIRO (Mb)
Waziri wa Katiba na Sheria


4.3.2 Naibu Waziri - Hakuna mabadiliko


4.4 WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI

Hakuna mabadiliko


4.5 WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA

4.5.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

4.5.2 Mhe. Janet Zebedayo MBENE (Mb)
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara


4.6 WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA

Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb)
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa


4.7 WIZARA YA UJENZI

Hakuna mabadiliko

4.8 WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

4.8.1 Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb)
Waziri wa Mambo ya Ndani

4.8.2 Naibu Waziri - Hakuna Mabadiliko



4.9 WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

4.9.1 Mhe. Dkt. Seif Seleman RASHIDI (Mb)
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii

4.9.2 Mhe. Dkt. Kebwe Stephen KEBWE (Mb)
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii


4.10 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

4.10.1 Waziri: Hakuna mabadiliko

4.10.2 Mhe. Jenista Joakim MHAGAMA (Mb)
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi


14.11 WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

14.11.1 Waziri: Hakuna mabadiliko

14. 11.2 Mhe. Dkt. Pindi Hazara CHANA (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto


14.12 WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

14.12.1 Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Dismas KAMANI (Mb)
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

14.12.2 Mhe. Kaika Saning’o TELELE (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi


14.13 WIZARA YA KAZI NA AJIRA

Hakuna mabadiliko

14.14 WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Hakuna mabadiliko
14.15 WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI

14.15.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

14.15.2 Mhe. George Boniface Taguluvala SIMBACHAWENE (Mb)
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi


14.16 WIZARA YA MAJI

14.16.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

14.16.2 Mhe. Amos Gabriel MAKALLA (Mb)
Naibu Waziri wa Maji

14.17 WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA

14.17.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

14.17.2 Mhe. Godfrey Weston ZAMBI (Mb)
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika


4.18 WIZARA YA UCHUKUZI

Hakuna mabadiliko


4.19 WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

4.19.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

4.19.2 Mhe. Juma Selemani NKAMIA (Mb)
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo


4.20 WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

4.20.1 Mhe. Lazaro Samuel NYALANDU (Mb)
Waziri wa Maliasili na Utalii

4.20.2 Mhe. Mahmoud Hassan MGIMWA (Mb)
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii

4.21 WIZARA YA NISHATI NA MADINI

4.21.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

4.21.2 Naibu Waziri (Madini) - Hakuna mabadiliko

4.21.3 Mhe. Charles Muhangwa KITWANGA (Mb)

Naibu Waziri (Nishati)

Itakumbukwa kwamba:
Rais Jakaya Kikwete, kwa kutangaza mabadiliko katika baraza lake la mawaziri inafuatia uteuzi wa mawaziri watatu kutenguliwa, mmoja kujiuzulu na mwingine kufariki dunia. Desemba 20, 2013. Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliwasilisha bungeni taarifa ya uchunguzi kuhusiana na athari zilizojitokeza katika Operesheni Tomokeza Ujangili iliyositishwa na serikali wakati wa Mkutano wa 13 wa Bunge kufuatilia malalamiko ya wananchi, wabunge na wadau.

Akiwasilisha ripoti hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli, alisema uchunguzi wao ulibaini kuwa operesheni hiyo iliendeshwa bila kufuata taratibu na matokeo yake kusababisha mateso kwa raia, vifo na upotevu wa mali hususani mifugo. Baada ya ripoti hiyo kuwasilishwa, wabunge walichachamaa na kushinikiza mawaziri ambao wizara zao zilihusika katika utekelezaji wa operesheni hiyo wawajibike kisiasa au wawajibishwe.

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, aliamua kujiuzulu wakati mjadala ukiendelea na siku hiyo baadaye Rais Kikwete, alikubaliana na mapendekezo ya wabunge kwa kutengua uteuzi wa mawaziri watatu, Dk. Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani ya Nchi); Mathayo David Mathayo (Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi) na Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na JKT). Januari Mosi, 2014, aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa, alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Kloof Medi-Clinic, Pretoria, Afrika Kusini na kuzikwa kijijini kwake Magunga, Jimbo la Kalenga, mkoani Iringa tarehe 6 Januari 2014.

MABADILIKO YA KWANZA

Rais Kikwete aliunda upya baraza lake la mawaziri Februari, 2008 baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujiuzulu kutokana na kuhusishwa na kashfa ya kuipa Kampuni ya Richmond Development Company LLC ya Houston, Texas nchini Marekani zabuni ya kufua umeme wa dharura wa megawati 100 kwa upendeleo. Lowassa alijiuzulu sambamba na waliokuwa mawaziri wawili Dk. Ibrahim Msabaha (Ushirikiano wa Afrika Mashariki) na Nazir Karamagi (Nishati na Madini). Karamagi na Dk. Msabaha, wote walikuwa wameiongoza wizara ya Nishati na madini kwa nyakati tofauti.

Hatua ya kujiuzulu kwa Lowassa na wenzake, ilitokana na ripoti ya Kamati teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, iliyowasilishwa bungeni baada ya kukamilisha kazi ya uchunguzi kujiridhisha kuhusiana na uhalali wa kampuni hiyo ndani na nje ya nchi. Kamati hiyo pia iliundwa na Stella Manyanya (Viti Maalum), Mohamed Mnyaa (Mkanyageni-CUF), aliyekuwa Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM) na Herbert Mntangi (Muheza-CCM), ambao wal; ibaini kuwa kampuni hiyo ilikuwa feki.

MABADILIKO YA PILI
Rais Kikwete alifanya mabadiliko ya pili katika baraza lake Mei, 2008 baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu na Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge. Chenge alichukua uamuzi huo baada ya kubainika kuwa anamiliki akaunti iliyokuwa na Dola za Marekani milioni moja (wakati huo Sh. bilioni 1.2) katika benki moja katika kisiwa New Jersey, nchini Uingereza. Akaunti hiyo ilibainiwa na wapelelezi wa Ofisi ya Upelelezi wa Makosa ya Ufisadi ya Uingereza (SFO) na kuhusishwa na fedha za kashfa ya ununuzi wa rada ya kijeshi ambayo Tanzania iliinunua kutoka Uingereza wakati huo Chenge akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali mapema miaka ya 2000. Ilidaiwa kuwa huenda Chenge alipata fedha hizo kutokana na rada hiyo kununuliwa kwa bei ya juu kuliko thamani yake. Baada ya Chenge kujiuzulu, nafasi yake ilichukuliwa na Mbunge wa
Bagamoyo, Dk. Kawambwa huku Rais Kikwete pia akibadilisha mawaziri kadhaa.

MABADILIKO YA TATU

Mei 2012, Rais Kikwete alifanya mabadiliko ya tatu katika baraza lake la mawaziri baada ya kuwaondoa mawaziri sita kufuatia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG), na kubaini mawaziri hao kwa nyakati tofauti walikiuka maadili ya utumishi wa umma na kushindwa kuwajibika kisiasa kusimamia mali za umma. Katika mabadiliko hayo, waliondolewa ni wa Mustafa Mkulo (Fedha); William Ngeleja (Nishati na Madini); Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii); Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii); Omari Nundu (Uchukuzi) na Dk. Cyril Chami (Viwanda na Biashara). Wengine waliotimuliwa ni Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Athumani Mfutakamba na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Lucy Nkya. Dk. Mponda na Dk. Nkya waliponzwa na mgomo wa madaktari.








All the contents on this site are copyrighted ©.