2014-01-15 09:40:04

Wayahudi na Wakatoliki; majadliano endelevu


Tarehe 16 Januari 2014 Kanisa Katoliki nchini Italia linaadhimisha Siku ya 18 ya Mwendelezo wa Majadiliano kati ya Wakristo na Wayahudi. Rabbi Abraham Skorka, Gombera wa Seminari kuu ya Marabbi wa Amerika ya Kusini, ameandaa mkutano unaofanyika kwenye Chuo Kikuu cha Kipapa cha Gregoriani, kilichoko hapa mjini Roma.

Itakumbukwa kwamba, Rabbi Skorka kutoka Buonos Aires ni mwandishi mwenza na Baba Mtakatifu Francis. Wao waliandika kitabu kinachojulikana kama "El cielo y la terra" "Mbingu na Dunia", ambacho ni mkusanyo wa tema mbali mbali zinazohusu tunu msingi za maisha ya binadamu, maadili na utu wema.

Mkutano huu unaangalia pamoja na mambo mengine: Majadiliano ya Kidini kati ya Wayahudi na Wakatoliki, Miaka 50 Baada ya Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican kuchapisha Hati ya Majadiliano ya Kidini, inayojulikana kwa Lugha ya Kilatini, "Nostra Aetate", Mwelekeo kutoka Amerika ya Kusini. Kardinali Kurt Koch, Rais wa Tume ya Kipapa ya uhusiano na Wayahudi.







All the contents on this site are copyrighted ©.