Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ameungana na Watanzania
na Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari
12, mwaka 1964. Mapinduzi hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania,
Hayati Abeid Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan
na kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengi kujitawala
ndani ya nchi yao wenyewe.
Yalikuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua
njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi
hayo – Aprili 26, 1964