Askofu mwandamizi Tsegaye Keneni ateuliwa kuwa Askofu wa Vikarieti ya Kitume ya Soddo,
Ethiopia
Baba Mtakatifu Francisko amekubali ombi la kung'atuka kutoka madarakani lililotolewa
na Askofu Rodrigo Meija Saldarriaga wa Vikarieti ya Kitume ya Soddo, nchini Ethiopia
kadiri ya sheria za Kanisa Namba 401, Ibara 1.
Wakati huo huo, Baba Mtakatifu
amemteua Askofu mwandamizi Tsegaye Keneni Derra kutoka Vikarieti ya Soddo, kuwa Askofu
wa Vikarieti ya Kitume ya Soddo, kuanzia tarehe 12 Januari 2014.