Inasikitisha kuona na kusikia nyanyaso na mauaji ya wazee kutoka sehemu mbali mbali
za dunia. Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya
kijamii anasema kwamba, hakuna sababu ya msingi ya kumfanya mzee yeyote yule kujisikia
kuwa uhamishoni katika familia. Wazee ni hazina muhimu sana katika Jamii.