SIGNIS kufanya mkutano wake mkuu mjini Roma, Februari 2014
Mwaka 2013 umekuwa ni mwaka uliosheheni matukio makubwa ya kihistoria. Mwezi Machi
Baba Mtakatifu Benedikto XVI akaamua kung’atuka kutoka madarakani kwa utashi wake
kamili, kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Kanisa la Kristo mchungaji mkuu. Makardinali
wakamchagua Kardinali Jorge Mario Bergoglio kutoka Argentina kuliongoza Kanisa Katoliki
kama Khalifa wa Mtakatifu Petro. Akachagua jina la Mtakatifu Francisko: fukara, mpenda
amani na mtunza mazingira.
Tangu alipochaguliwa,
Baba Mtakatifu Francisko ameonesha upendeleo wa pekee kwa maskini na wote wanaosukumizwa
pembezoni mwa Jamii si tu kwa maneno bali hata kwa mtindo wake wa maisha. Tarehe 17
Desemba, 2013, Kanisa linakungana na watu wenye mapenzi mema kuadhimisha kumbu kumbu
ya miaka 77 tangu Baba Mtakatifu Francisko alipozaliwa.
Hivi ndivyo anavyoandika
Bwana Augustine Loorthusamy, Rais wa Shirikisho la Vyama vya Mawasiliano ya Kanisa
Katoliki Duniani, katika salam zake za Noeli ina Mwaka Mpya 2014. Anasema, Juni 2013,
Sigins ilifuta mkutano mkuu wa Mwaka uliokuwa ufanyike mjini Beiruti, hapo Mwezi Oktoba,
2013 kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria. Hali bado ni tete kwani
kuna mateso na mahangaiko mengi ya watu wasiokuwa na hatia nchini Syria na Ukanda
wa Mashariki katika ujumla wake.
SIGNIS baada ya tafakari ya kina, imeamua
kufanya mkutano wake mjini Roma, hapo mwezi Februari 2014. Hii inatokana na ukweli
kwamba, lisingekuwa ni jambo la busara kukaa na kuendelea kusubiria tena kwa kipindi
cha miaka mingine minne bila ya kukutana. Uamuzi huu unazingatia changamoto mbali
mbali zinazoendelea kujitokeza katika ulimwengu wa maendeleo ya sayansi na teknolojia
ya habari. Mkutano huu utakuwa ni fursa ya kuchagua viongozi waandamizi wa SIGNIS
pamoja na kuweka dira na mwongozo wa SIGNIS kwa miaka ijayo.
Rais wa SIGNIS
anawaalika wajumbe kuhakikisha kwamba, wanashiriki kikamilifu katika maandalizi na
hatimaye, Maadhimisho ya Mkutano mkuu hapo Mwezi Februari, 2014. Anawatakia wanachama
wote kheri na baraka, amani na maendeleo kwa Noel ina Mwaka Mpya 2014.