2014-01-08 16:00:32

Ole wangu kama sitaihubiri Injili : Papa aonya.


Kazi ya Uinjilishaji ni wajibu wa Kanisa zima na watu wote wa Mungu .Hivyo Wakritu wote wameitwa kufanikisha utume huu wa kanisa. Papa Francisko ameandika katika ujumbe wake kwa ajili ya Mkutano wa Kitaifa wa 13, unaokutanisha jumuiya zote msingi mahalia za Kikanisa nchini Brazil.
Mkutano huo ulianza Jumanne mjini Juazeito de Norte , ukiongozwa na Mada Kuu "Haki na Unabii katika huduma ya maisha ", na unakamilika tarehe 11 Januari . Katika ujumbe huo, Papa amesisitiza kwamba, waamini wote wanapaswa kutembelea maeneo yote ya vijijini na mijini pia, kuipeleka furaha ya Injili, kwa kila binadamu, mwanamme na mwanamke .
Papa, amewakabidhi washiriki wa mkutano huo katika ulinzi wa Mama yetu wa Aparecida ,huku akisistiza kwamba, Jumuiya msingi mahalia , ni muhimu katika kazi msingi za Utume wa Kanisa. Na kwamba, Mara nyingi , kama alivyoeleza katika waraka wake wa Evangelii Gaudium, katika himizo jipya la Kuinjilisha, na juu ya uwezo wa mazungumzano na ulimwengu katika kulifanya upya Kanisa.

Na pia kama alivyoonya katika waraka wake wa kwanza wa kitume wenye kuwa na utajiri mkubwa wa ushauri, kwamba, jumuiya msingi mahalia hazipaswi kupoteza mahusiano yake na utajiri wa parokia mahalia , ambazo huchanganyika na vyombo vya kichungaji vya kanisa kwa namna ya kipekee.

Mwisho Papa ametoa wito kwa washiriki wa Mkutano kwa onyo la Mtume Paulo kwa Wakoritho: " Ole wangu kama sitaihubiri injili.








All the contents on this site are copyrighted ©.